Msako mkali dhidi ya makanisa ya kikristo umeanza China na kuzua taharuki

In Kimataifa

Hatua ya hivi karibuni ya msako mkali unaotekelezwa na polisi dhidi ya makanisa nchini China umesababisha taharuki kubwa kwamba serikali ya nchi hiyo inaonesha ubabe wake wa kuwakandamiza Wakristo.

Miongoni mwa waliokamatwa ni kasisi mmoja maarufu pamoja na mkewe. Wote ni wamiliki wa kanisa la Early Rain Covenant lililoko katika jimbo la Sichuan. Wawili hao wanashtakiwa kwa kosa la kuhujumu utendakazi wa serikali ya kikomunisti ya China na kwenda kinyume na maadili ya Wachina.

Juamamosi asubuhi, kikosi cha polisi kilivamia darasa moja la kidini lililokuwa likiwapa mafunzo watoto ndani ya kanisa la Rongguili huko Guangzhou.

China ni nchi isiyomuamini Mungu, japo mamlaka zinazesa zinatoa uhuru wa kuabudu.

Lakini kwa miaka mingi utawala wa nchi hiyo umechukua hatua dhidi ya viongozi wa kidini, ambao wanaonekana kutishia mamlaka au kuyumbisha uongozi wa taifa, ambayo kwa mjibu wa shirika la Human Rights Watch, “”Hufanya kejeli kwa madai ya serikali kwamba inaheshimu imani za kidini”.

Serikali inawashinikiza wakristo kujiunga na mojawepo ya makanisa makubwa matatu inayoonyesha uzalendo kwani zimepigwa msasa na serikali pamoja na chama tawala cha Kikomunisti, huku yakiongozwa na makasisi walioidhinishwa na serikali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu