Achimba kaburi ndani ya chumba cha kulala.

In Kimataifa


Jamaa mmoja wa miaka 25 kutoka kaunti ya Narok nchini
Kenya amewaacha watu vinywa wazi baada ya kuchimba kaburi
katika chumba chake cha kulala.


Kisa hicho cha kushangaza kilipelekea wakazi wa eneo hilo
kufurika nyumbani kwake Geoffrey Lang’at wakitaka kujua ni
kwa nini alichukua hatua kama hiyo.


Kulingana na jamaa huyo kaburi hilo lilikuwa ni lake na
hakuelewa ni kwa nini watu walijihusisha na maisha yake.
Wakati wakazi hao wakizidi kuulizana maswali jamaa huyo
alitoweka ghafla kijijini hapo na haijulikani alikoenda.


Mkewe amesema kuwa Mumewe alimwambia alikuwa akijenga
chumba kingine cha ardhini ndani ya chumba chake cha kulala.
Mwenyekiti wa Nyumba Kumi eneo hilo alithibitisha kisa hicho
na kusema kwamba tayari uchunguzi wa kumsaka Lang’at
umeanza.

Wazee wa mtaa wametangaza mpango wa kufanya tambiko za
kulitakasa boma la jamaa huyo kulingana na mila na tamaduni
za jamii ya Kipsigis.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu