Watu arubaini na moja wameuawa baada ya ndege ya Urusi kutua kwa dharura na kulipuka moto katika uwanja wa ndege wa Sheremetyevo mjini Moscow.
Video katika mitandoa ya kijamii zinaonyesha baadhi ya abiria wakitumia mlango wa dharura na kutoka kwenye ndege hiyo ya Aeroflot iliyokuwa inateketea moto.
Watoto wawili na mhudumu mmoja ni miongoni mwa waliofariki kwa mujibu wa vyombo vya habari Urusi.
Shahidi mmoja amesema ilikuwa ni “miujiza” kwamba kuna aliyenusurika mkasa huo wa ndege, iliyokuwa imebeba abiria 73 na maafisa wataano wa ndege.
“Watu 37 wamenusurika – Abiria 33 na maafisa wanne wa ndege hiyo,” amesema afisa wa kamati ya uchunguzi, Yelena Markovskaya.