Chama tawala cha Afrika Kusini (ANC) kimekanusha taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari kuwa rais Jacob Zuma atajiuzulu Kesho, Jumamosi na kusema taarifa hizo siyo sahihi na ni za kupotosha.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya mratibu mkuu wa chama hicho kwenye Bunge imesema, Chama cha ANC hakihusiki na taarifa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Cyril Ramaphosa amekiambia kikundi cha uongozi wa Bunge kuwa rais Zuma atajiuzulu Jumamosi na hatapewa kinga.
Mapema jana, vyombo vya habari vya Afrika Kusini viliripoti kuwa, Ramaphosa alikiambia kikundi cha uongozi cha Bunge kuwa kinga kwa rais Zuma siyo sehemu ya mjadala huo.
Ripoti hizo zilitolewa baada ya Ramaphosa kuwataka wananchi kutulia wakati wakijadili masuala husika na rais Zuma.