(ANC) wakanusha Kung’atuka kwa Zuma.

In Kimataifa

Chama tawala cha Afrika Kusini (ANC) kimekanusha taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari kuwa rais Jacob Zuma atajiuzulu Kesho, Jumamosi na kusema taarifa hizo siyo sahihi na ni za kupotosha.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya mratibu mkuu wa chama hicho kwenye Bunge imesema, Chama cha ANC hakihusiki na taarifa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Cyril Ramaphosa amekiambia kikundi cha uongozi wa Bunge kuwa rais Zuma atajiuzulu Jumamosi na hatapewa kinga.

Mapema jana, vyombo vya habari vya Afrika Kusini viliripoti kuwa, Ramaphosa alikiambia kikundi cha uongozi cha Bunge kuwa kinga kwa rais Zuma siyo sehemu ya mjadala huo.

Ripoti hizo zilitolewa baada ya Ramaphosa kuwataka wananchi kutulia wakati wakijadili masuala husika na rais Zuma.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu