Klabu ya Manchester City imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa mabao 3 – 0 dhidi ya Arsenal mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza uliyopigwa katika dimba la Emirates.
City inafanikiwa kuchomoza na ushindi huo kwa mara ya pili mfululizo baada ya wiki iliyopita kushuhudiwa timu hiyo ikinyakuwa kombe la Karabao Cup kwa ushindi kama huo mbele ya the Gunners.
Baada ya matokeo hayo meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa wachezaji wake walikosa kujiamini na ndiypo sababu ya kupoteza mchezo huo na kuwataka kuwa na umoja na kufikiria mchezo ujao.
Wakati imani yako inapokuwa ndogo cha kwanza kinachotokea kukosa kujiamini na nguvu kupungua na hicho ndicho kilichotokea katika mchezo.
Nadhani umeweza kuona usiku wa leo, sidharau ubora waliyokuwa nao City lahasha lakini tunapitia katika kipindi kigumu ndani ya uwanja.
Hii ni sehemu ya mchezo nilazima tuunganishe nguvu zetu na tuwe kitu kimoja ndani ya timu na tufikirie mchezo ujao na tuweke juhudi zetu huko.
Picha zinazo onyesha matukio mbalimbali uwanjani