Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Koplo Denis Minja
aliyemuokoa mtoto eneo la Murugwanza Wilayani Ngara
kwenye shimo la choo mwezi Mei mwaka huu,amemuokoa
mtoto mwingine jana Desemba 28-2020 huko Kata ya Kayanga
Tarafa ya Bugene Wilayani Karagwe.
Kwa mujibu wa Mkuu wa zimamoto na Uokoaji mkoa wa
Kagera, Inspekta Shaban Hamis Dawa amesema kuwa mtoto
huyo aitwaye Anekius Evarist miaka 2 alimfata mama yake
aliyeingia bafuni linalokaribiana na choo ila mtoto huyo aliingia
chooni akidhani mama yeke naye yupo chooni.