Atletico yapinga Barca kumnyakua Antoine Griezmann.

In Kimataifa, Michezo

Atletico Madrid imepinga kitendo cha Barcelona kumsajili Antoine Griezmann kinyume cha sheria za usajili.

Barcelona ilidai jana imemnyakua Griezmann baada ya kulipa pauni milioni 108 (Sh. bilioni 310) kama ilivyokuwa inaelekezwa kwenye mkataba baina ya Griezmann na Atletico.
Kifungu hicho kinatoa ruhusa kuanzia Julai Mosi kwa timu yoyote yenye pauni milioni 108 kutoa fedha hizo na kumchukua mchezaji huyo. Kutokana na Atletico kugoma kupokea fedha basi Barcelona walichukua uamuzi wa kulipa fedha hizo kwenye Shirikisho la Soka Hispania kama kanuni inavyotaka.
Rais wa Atletico Madrid, Enrique Cerezo amedai kuwa Barcelona wanapaswa kulipa kiasi cha pauni milioni 180 (Sh. bilioni 517) kwa kuwa walivunja kanuni za usajili kwa kuzungumza na mchezaji mwenyewe tangu Machi wakati wakiwa na mkataba naye.

 

Aliongeza kuwa, watapeleka suala hilo kwenye Shirikisho la Soka Hispania na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA). Cerezo alisema kuwa wamechukizwa na tabia ya Griezmann kwa kuikosea heshima klabu aliyochezea kwa miaka mitano.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu