Baada ya kufungiwa, Wambura aibua mapya TFF.

In Kitaifa, Michezo
Ukimwaga mboga, namwaga ugali ni miongoni mwa misemo maarufu ya lugha ya Kiswahili ambao unaweza kutimia baada ya Makamu wa Rais wa TFF kufungiwa maisha kujihusisha na masuala ya soka kufuatia kutiwa hatiani na kamati ya maadili ya TFF.
Baada ya hukumu kutangazwa, Michael Wambura alizungumza na vyombo vya habari akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo lakini amesema kufungiwa kwake ni kwa hila na njama iliyopangwa na watu wachache.
Wambura ameibua hoja kadhaa akiituhumu TFF kuajiri baadhi ya watu bila nafasi hizo kutangazwa kama taratibu na kanuni zinavyoelekea, lakini pia ameituhumu tff kutumia kiasi kikubwa cha pesa kwa muda mfupili lakini hakuna kinachoonekana kufanywa kulingana na kiasi hicho cha pesa.
“Ni kweli kulikuwa na kikao lakini bado nasisitiza kilikuwa cha hila kilikuwa ni kikao ambacho kimeandaliwa kwa ajili ya kutoa maamuzi bila kujali hoja ambazo zitakwenda kujadiliwa. Ninasema hivyo kwa sababu siku ya Jumatatu nilikuwa TFF niliongea na Rais wa TFF pamoja na Katibu, Jumanne niliongea na Rais wa TFF lakini wote hawakuniambia kama kuna jambo lipo TFF linanihusu mpaka Jumanne nasafiri hakuna chochote kutoka TFF kuja kwangu lakini jioni saa 12 wanakwenda nyumbani kwangu kupeleka mashtaka.
“Kwa hiyo tayari kuna hila ambazo nilikuwa nimeziona katika jambo hilo, katika mashtaka yao msingi mkuu umeegemea katika kufoji document hakuna anaebisha walikuwa hawadaiwi, wote wanakiri kudaiwa katika barua mbalimbali za TFF lakini wanasema kwamba document zimefojiwa.
“Kiutaratibu kuna njia mbili, njia moja ni kupeleka polisi wakaangalie kama document imefojiwa baada ya kupata majibu ya polisi mnaelekea katika mkondo washeria ndio msingi wa hizi kamati. Hizi kamati haziwezi kuingia mahali ambapo kosa ni la jinai, ufojaji ni kosa la jinai sio la kimaadili kwa hiyo ilipaswa iende katika mfumo wa sheria ya jinai sio mfumo wa kimaadili.
“Kampuni ambayo wanasema document yake imefojiwa ilipaswa iitwe kwa sababu kampuni inaishi na ina wakurugenzi, kwa hiyo wakurugenzi ndio walipaswa kuitwa ikishajulikana hivyo kinachofuata ni kupelekwa polisi na kushtakiwa kama mhalifu mwingine lakini kwa sababu wameona hawana kesi ya msingi wakaamua kukaa na kamati walizoziunda wenyewe ili wamtoe Wambura katika nafasi kitu ambacho hakikubaliki.
“Kwa hiyo ninachoona yote haya ni kutokana na matatizo yaliyopo ndani ya TFF, jambo la miaka 14 iliyopita unataka kulijadili kwa siku moja kwa kumpa mtu notice usiku asubuhi aje mbele ya kamati, viongozi walikuwepo wengi wamepita hapo katikati wote walitakiwa waje kutoa ushahidi lakini hawakuitwa? Kwa nini walilipa? Au aliyelipwa alivunja ofisi?
“Isije ikawa kuna mtu amejilipa ndani ya TFF kwa jina la ile kampuni na kitu ambacho kipo, kuna watu wamelipwa pesa kwa kutumia jina la hiyo kampuni wakati hizo pesa hazijalipwa kwa kampuni ndiyo maana wanashindwa kutoa hizo document ndiyo maana tunasema walete nyaraka za hayo malipo kama hawajaiba wao wenyewe wanashindwa.
“Kama wanasema nimefoji barua nipo tayari twende polisi na mahakamani ndio maana nasema hili jambo limetengenezwa kimkakati halina mashiko hata kidogo ya kisheria, halina ushahidi ni jambo la uongo na kizandiki limetengenezwa na kikundi cha watu ambao wanaamini nikitoka kama mwenyekiti wa fedha mambo yao yatakuwa mazuri.
“Mimi nimechaguliwa na mkutano mkuu kwa zaidi ya kura asilimia 80, siwezi kuondolewa na watu watatu ambao hawakuchaguliwa hawana dhamana ya mkutano mkuu, haiwezekani. Kama unadhani nina kosa kanishtaki kule.
“Ni kweli kwamba kila uongozi unapokuja unakuwa na taratibu zake , sisi taratibu zetu za kiutendaji ni kwamba, nafasi ya katibu mkuu wa TFF lazima itangazwe kama makatibu wakuu wengine walivyopita, nafasi inatangzwa watanzania wenye sifa wanaomba kupitia makampuni ambayo ni huru, wanafanya usaili wanaajiriwa.
“Sisi pale kwetu kuna shida kidogo kuna watu wengine bado wana kazi mbili, kuna mtu mwinngine ameajiriwa huku anakuja pale kama secondment wakati kuna watanzania wengi wanaweza kuomba na kuajiriwa, sasa mtu ana kazi mbili.
“Suala la katibu mkuu anapaswa kuajiriwa, tulipochaguliwa kaimu katibu mkuu alikuwa Salum Madadi kwa sababu madadi alikuwa majiriwa wa TFF kwa hiyo alikuwa anakaimu nafasi kwa sababu alikuwa mwajiriwa wa TFF baadaye tulipokuja kumpa nafasi Wilfred Kidao yalikuwa ni makosa kwa sababu sheria zinakataza mjumbe wa mkutano mkuu kuajiriwa TFF na kidao ni mwenyekiti wa TAFCA hawezi kuajiriwa akawa mjumbe wa mkutano mkuu wakati huohuo.
“Tuna matatizo mengi, TRA wanatudai lakini bado tunakusanya kodi na tunazitumia, tunamatatizo ya fedha za wafadhili tunazihamisha matokeo yake ligi ya wanawake inasimama, wakati mwingine hata ligi kuu inasimama kwa sababu hakuna pesa lakini Azam wamelipa kwa hiyo tuna shida.
“Tunaposema tunataka tuweke nyumba kwenye mstari masuala ya kodi yaeleweke kodi zinazopokelewa na bodi zikalipwe TRA badala ya kuletwa TFF ndio mgogoro unapotokea. Bodi ya ligi ina kusanya kodi toka Azam, na wadhamini mbalimbali lakini kodi zile zinakuja kwetu TFF zikishakuja na kutumika mwenyekiti wa kamati ya fedha akisema hapana sio sahihi inakuwa issue.
“Matatizo mengi tutakuja kuyaona siku chache zijazo, watanzania watanielewa kwamba ndani ya TFF kuna matatizo makubwa sana na sio madogo kama watu wanavyofikiria, siku chache zijazo tutakuja kuyazungumza.
“Tumeshatumia kiasi cha shilingi 3 bilioni ndani ya miezi nane, kuna nini tumefanya? Zinapita tu. Jambo moja linapoanza uzuri wake linafuata na jingine kwa hiyo tutakwenda mpaka mahali tutakuwa sawa na ninaamini watafuata ninachokisema, bado tunahitaji kusafisha TFF kwa sababu haiko sawa.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu