Baada ya kupata mtoto wa tatu, Messi apewa zawadi ya kipekee na FC Barcelona

In Kimataifa, Michezo

Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi jana Machi 10, 2018 amepata mtoto wa tatu wa kiume aliyebatizwa kwa jina la Ciro.

Messi na familia yake wakiwa na Ciro

Kufuatia ushindi huo klabu ya Barcelona ambayo usiku wa kuamkia leo imepata ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Malaga, Kocha wa klabu hiyo, Ernesto Valverde amesema kuwa zawadi pekee ya Messi ni ushindi huo waliyoupata jana usiku kwani hakuna zawadi ambayo ingekamilisha furaha ya mchezaji huyo.

Nimeongea na Messi baada ya mchezo kumalizika, amesema anajiona mtu mwenye furaha zaidi kwa siku ya leo kwani mbali ya kupata mtoto lakini amefurahishwa zaidi na matokeo. Napenda kusema kuwa ushindi huu ni zawadi yake, hakuna zawadi nyingine kubwa kwa mchezaji wa Barcelona zaidi ya ushindi,“amesema Ernesto Valverde.

Mabao ya Barcelona yamefungwa na Luis Suarez dakika ya 15, na Philippe Coutinho, dakika ya 28 na kuifanya klabu hiyo kujikita kileleni kwa alama 72.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu