Babalevo kuminyana na Zitto Ubunge

In Kitaifa, Siasa

Msanii Babalevo ambaye ni diwani aliyemaliza muda wake katika kata ya Mwanga Kaskazini Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia chama cha ACT wazalendo, amesema sasa anakwenda kugombea ubunge.

Msanii wa Bongo Fleva na Diwani mstaafu, Babalevo amesema ni muda sasa wa kuwania ubunge na atakwenda kugombea katika jimbo la Kigoma Mjini.

”Baada ya hapa naondoka naelekea Kigoma kwa wananchi wangu nakwenda kuchukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Kigoma Mjini kama Mh Zitto hatagombea lakini akigombea nitaenda jimbo jingine”, amesema.

Babalevo amehudumu kama diwani wa Mwanga Kaskazini kwa miaka mitano lakini pia amewahi kutumia kifongo jela, ambapo mwenyewe anasema jela ilimfundisha mambo mengi ikiwemo kumjua Mungu.

Kwa upande mwingine Babalevo amesema akipata kiinua mgongo chake cha Mil 20 au zaidi basi Mil 10 atazirudisha kwa wananchi wake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu