Bangi sasa ruksa Canada.

In Kimataifa

Canada imepitisha sheria rasmi kwa nchi nzima inayoruhusu matumizi ya bangi hadharani tofauti na hapo awali ambapo iliwabidi wananchi kutumia kwa kujificha.

Sheria hiyo hatimaye ilishinda kwa kupata kura za ndiyo 52 zinazoruhusu matumizi ya bangi hadharani, huku kura 29 za maseneta zikisema hapana Sheria hiyo inasimamia udhibiti, usambazaji na uuzaji wake.

Aidha, kwasasa raia wa Canada wataruhusiwa kununua na kutumia bangi kihalali kuanzia mwezi Septemba mwaka huu.

Kumiliki bangi ilikuwa ni kosa kisheria tangu mwaka 1923 lakini matumizi ya bangi kama dawa yaliruhusiwa kisheria tangu mwaka 2001.

Vile vile kutokana na kupitishwa kwa sheria hiyo sasa itayalazimu Majimbo, Manispaa na Mamlaka kutengeneza masoko mapya ya kuuza bangi.

Hata hivyo, Umri unaoruhusiwa kununua na kutumia bangi umepitishwa kwa mjibu wa sheria hiyo kwamba ni kuanzia miaka 18, lakini baadhi ya majimbo yamependekeza umri wa kuanzia miaka 19.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu