Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limewataka watumishi wote wenye malalamiko kuhusu uhakiki wa vyeti vyao kupeleka malalamiko yao kwa Katibu Mkuu ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

In Kitaifa

SIKU chache baada ya kuwekwa hadharani majina ya watumishi walioghushi vyeti na wenye malalamiko kuanza kumiminika katika ofisi za Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), kutaka ufafanuzi wa uhakiki wa taarifa zao, baraza hilo limewataka watumishi hao kupeleka kwa maandishi malalamiko yao kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Pamoja na Necta kuwataka watumishi hao kwenda kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, walipofika katika ofisi hizo, malalamiko yao hayakupokelewa, kwa kile walichoelezwa kuwa NECTA inapaswa kuwapa taarifa ya nini cha kufanya na hawakuwa na taarifa hiyo bado mpaka jana.

Hata hivyo wakati hayo yakijiri, Waziri katika Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki, alipoulizwa kuhusu suala hilo, alilieleza gazeti hili mjini Dodoma jana kuwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, atalitolea ufafanuzi leo mjini humo.

Hivi karibuni Rais, John Magufuli alikabidhiwa taarifa ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma ambapo watumishi zaidi ya 9,932 walibainika kuwa na vyeti vya kughushi na alitangaza kuwafuta kazi na aliwapa siku 15, wawe wameondoka kazini, la sivyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma, alichapisha sehemu ya kwanza majina ya watumishi hao katika vyombo vya habari na jana baadhi ya watumishi walianza kumiminika katika ofisi za Necta, kutaka kujua kasoro za vyeti vyao.

Katika kushughulikia tatizo hilo, Baraza hilo kupitia kwa Katibu Mtendaji wake, Dk Charles Msonde limewataka watumishi wa umma wenye malalamiko kuhusu matokeo ya uhakiki wa vyeti vyao, wawasilishe malalamiko yao kwa maandishi kwa Katibu Mkuu Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia kwa waajiri wao na barua hizo za malalamiko, ziambatanishwe na nakala za vyeti husika.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu