Baraza la Seneti lapitisha Mswada wa kuwawekea vikwazo Urusi, iran na korea Kaskazini

In Kimataifa

Baraza la Seneti la Marekani kwa sauti moja hapo jana limepitisha mswada wa kuziwekea vikwazo vipya Urusi, Iran na Korea Kaskazini, na kuuwasilisha mswada huo kwa Rais Donald Trump ambaye sasa anatakiwa kufanya uamuzi wa kutia saini ili ugeuke kuwa sheria.

Mswada huo unamzuia rais Trump kuipunguzia vikwazo Urusi bila ya idhini ya seneti.

Trump amekuwa akisisitiza mara kwa mara juu ya kuwepo kwa uhusiano mzuri na Urusi, licha ya uchunguzi uliofanywa mara kadhaa kuhusu Urusi kuingilia uchaguzi wa rais wa mwaka jana uliomuweka Trump madarakani.

Vikwazo dhidi ya Korea ya Kaskazini vinalenga silaha zake za nyuklia na mpango wake wa makombora na Iran inalengwa kwa shughuli zake za kigaidi, ukiukwaji wa haki za binadamu pamoja na mipango ya makombora ya masafa marefu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu