Benki Kuu yapunguza riba kwa mabenki ya baishara, ni neema kwa watanzania wa chini

In Kitaifa, Uchumi

Benki kuu Tanzania imepunguza kiwango cha riba kwa mabenki ya biashara kufikia asilimia 11.

Hatua hiyo inadaiwa itawezesha mabenki ya biashara kupunguza gharama za kukopa fedha benki kuu hivyo kutoa uwezekano wa kupunguza riba kwa wateja wao pia serikali ilichukua hatua ya kupunguza kiasi cha fedha ambacho mabenki ya biashara ilikuwa ikitunza Benki Kuu(Statutory minimum reserve ratio) kutoka asilimia 10 mpaka nane ili kuziwezesha benki kuwa na fedha zaidi kwa ajili ya kukopesha.

Katika hatua nyingine, riba za dhamana za serikali zimepunguzwa kufikia wastani wa asilimia sita, hatua hiyo itapunguza mabenki kufanya biashara na serikali na badala yake kuwakopesha watu wa kawaida kutokana na faida ya kuikopesha serikali kuwa ndogo sana ukilinganisha na kukopesha watu wa kawaida.

Naibu gavana wa Benki kuu, Dr. Kibesse amesema benki kuu imekuwa ikichukua hatua hizo ili kuwawezesha wananchi wamudu kukopa ndio maana kiwango cha riba kimekuwa kikishuka.

Akiwa kwenye kikao na wafanyabiashara Ikulu Juzi, Rais Magufuli alielezea azma ya serikali kufanya fedha yake kuwa ngumu kwa mabenki ili warudi kwa wananchi ikiwemo kupunguza kutoa hati fungani za serikali kwa mabenki

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu