Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema uamuzi uliofanywa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kuhamia Chama cha ACT- Wazalendo, umeonyesha na kuthibitisha kwamba utawala uliopo unaozingatia misingi ya Katiba ambayo CCM imeutekeleza.
CCM ilitoa kauli hiyo kupitia kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole , baada ya Maalim Seif kutangaza kuhamia ACT- Wazalendo, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutoa hukumu yake kumtambua Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti halali wa CUF.
Pole pole amesema kuwa huu ni Utawala wa sheria unaoruhusu mihimili ya dola kufanya kazi pasina kuingiliwa, watu wanazo haki kufanya uamuzi wa kisiasa kwa kujiunga na chama chochote.