–
Taratibu za uokoaji zinaendelea huko Sichuani Kusini Magharibi mwa China baada ya kutokea tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6 Kipimo cha Richa, jana usiku
–
Baada ya tetemeko hilo, usiku huo huo kulitokea tetemeko jingine lenye ukubwa wa 5.1 Kipimo cha Richa na asubuhi ya leo limetokea tena ingawa halikuwa kubwa
–
Kwa mujibu wa Wizara ya Kupambana na Majanga ya Dharura imesema majengo 73 yameharibiwa ikiwemo hospitali katika Kaunti ya Changning na wagonjwa wamehamishiwa hospitali nyingine
–
Aidha, Waokoaji wamefanikiwa kuokoa watu 8 asubuhi ya leo waliokuwa wamenasa kwenye vifusi vya majengo yaliyoanguka