Dada yake Rais Magufuli aaga dunia.

In Kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefiwa na dada yake, Monica Joseph Magufuli aliyekuwa amelazwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza.

Monica amefariki leo August 19 ikiwa ni siku moja tangu Rais Magufuli amtembelee katika chumba cha uangalizi maalum hospitalini hapo.

Akitoa taarifa hiyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa kupitia akaunti zake za kijamii ameandika ujumbe ukiambatana na picha ya dada huyo wa Rais Magufuli akisema;

“Nasikitika kuwajulisha kuwa Dada wa Rais (John Magufuli), Monica Joseph Magufuli amefariki dunia leo Agosti 19, 2018 katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza alikokuwa akipatiwa matibabu,” amesema Msigwa.

“Natoa pole kwa Rais John Pombe Joseph Magufuli, familia ya Mzee Joseph Magufuli, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huu,” ameongeza.

Msigwa amemaliza kuandika ujumbe wake akisema;

“Raha ya milele umpe e Bwana na mwanga wa milele umuangazie, marehemu Monica Jospeh Magufuli astarehe kwa amani, Amina.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu