Deni lasababisha ATCL kufungiwa.

In Kitaifa

Shirika la Ndege nchini ATCL limeondolewa katika mfumo wa malipo wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga IATA kutokana na kukabiliwa na madeni na sasa limetia saini makubaliano ya miaka mitano na Kampuni ya Ndege ya HAHN Air kuuza tiketi za Air Tanzania.

Akizungumza na Waandishi wa habari visiwani Zanzibar, Mkurugenzi wa ATCL Ladislaus Matindi amesema wamelazimika kuingia makubaliano na kampuni hiyo ili wasikose baadhi ya huduma ya malipo ya tiketi.

“Sikumbuki yalifikia kiasi gani lakini ni madeni makubwa, ambayo yalisababisha siye kusimamishwa uanachama au kufungiwa huduma hizi mpaka tutakapokuwa tumelipa hayo madeni” -Matindi

“Kubwa zaidi ilikuwa ni sisi kuwa katika mfumo wa Shirikisho la Mashirika ya ndege ya Dunia IATA, ambao kwa kweli ni sehemu mojawapo ya huo mfumo wote wa utawanyaji na uuzaji wa ticket, maana mabadilishano ya pesa au upelekaji wa pesa kutoka shirika moja kwenda lingine upitia IATA, ni kupitia mgongoni kwa mtu, lazima tutoe madeni yetu tuliyonayo IATA na ni Mabilioni” -Matindi

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu