Mkurugenzi msaidizi kitengo cha ufuatiliaji wa Magonjwa ya
mlipuko Dkt Janeth Mghamba,ameeleza kuwa dereva aliyekuwa
amembeba muathika wa kwanza wa Corona nchini Bi Isabella
Mwampamba,vipimo vimeonyesha hana virusi vya Corona.
Mbali na dereva huyo pia Dkt Janeth Mghamba amesema kuwa,
wale wote walikuwa katika mtandao uliomhusisha Dereva huyo
pia hawajapatikana na ugonjwa huo.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo
amesema kuwa mkoa wa Arusha ni Shwari na dereva taxi aliyembeba Mgonjwa wa Kwanza wa Korona amekutwa hana Maambukizi ya Virusi vya Corona