Donald Trump Junior akubali kufanyiwa mahojiano na kamati ya senate ya Marekani

In Kimataifa

Gazeti la New York Times limeripoti kuwa mwanawe Rais wa Marekani Donald Trump, Donald Trump Junior amefikia makubaliano na kamati ya ujasusi ya baraza la senate la Marekani kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano na jopo la kamati hiyo katikati ya mwezi Juni. Likimnukuu mtu ambaye alifahamishwa kuhusiana na makubaliano hayo gazeti hilo limesema kikao hicho cha faragha kitajumuisha maswali kuhusu mada sita na kitadumu kwa chini ya saa nne. Kamati hiyo ya seneti inayoongozwa na wabunge wa chama cha Republican ilikuwa imemuita Donald Trump Junior wiki iliyopita kuhudhuria kikao hicho ili ajibu maswali kuhusiana na maafisa wa Urusi aliowasiliana nao. Ushahidi wa kwanza alioutoa Trump Junior mbele ya kamati hiyo ulikuwa kuhusu ushiriki wake katika mkutano wa mwezi Juni mwaka 2016 katika jengo la Trump Tower ambapo alikutana na raia wa Urusi waliompa taarifa kuhusu mgombea wa Urais wa chama cha Democratic wakati huo Hillary Clinton aliyekuwa anashindana na Donald Trump.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu