Drake kuhama Nike na bidhaa zake za Jordan kwenda Adidas.

In Burudani, Kimataifa

Siku zote ukiwa maarufu na jina lako ukiweza kulitumia vizuri utaweza kupata dili nyingi kutoka makampuni mbali mbali, moja likiona haufai basi kuna wengine wanatamani kufanya kazi na wewe, na fursa ni kama kiti cha daladala ya Makumbusho-Posta, akishuka mmoja mwingine anakaa.

Imedaiwa kuwa Drake anampango wa kuhamishia bidhaa zake za brand yake ya Jordan na kupeleka katika kampuni ya Adidas.

Drake ambaye amekuwa akifanya kazi kwa pamoja ya utengenezaji wa bidhaa zake hizo na Nike tangu Disemba 2013, amedaiwa kutokuwa na furaha na ushirika wake wa sasa na Nike na anaangalia njia ya kuondoka ili kupata uwezo zaidi wa ubunifu chini ya kampuni ya adidas.

Endapo Drake atajiunga na Adidas atakuwa ameungana na mastaa wengine kama Pharrell Williams na Kanye West ambaye lisababisha Drizzy apate dili na kampuni ya Nike mwaka 2013.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu