Fuvu la binadamu wa kale linalotarajiwa kuoneshwa hadharani kwa mara ya kwanza tangu ligunduliwe kuongeza idadi ya watalii Ngorongoro.
Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii Prof. Adolph Mkenda amesema kuwa fuvu la binadamu wa kale zinjanthropus linalotarajiwa kuoneshwa hadharani kwa mara ya kwanza tangu ligunduliwe mwaka 1954 katika makumbusho ya Oldvai wiilayani Ngorongoro litatumika kuhamasisha utalii wa ndani na nje ili kuongeza idadi ya watalii kutokana kuwa kiwakilishi muhimu katika historia ya binadamu duniani.