Naibu Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi na Mbunge wa
Jimbo la Kikwajuni Unguja, Hamadi Yusuf Masauni
amajitokeza kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Urais wa
Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM.
Mhandisi Masauni anakuwa mgombea wa 19 kufika katika ofisi
kuu za Chama cha Mapinduzi CCM Kisiwandui Mjini Unguja
kwa ajili ya kuchukua fomu hizo za kugombea nafasi ya Urais.