Hamas yatangaza kusitisha mapigano.

In Kimataifa

Chama cha Wapalestina cha Hamas kinachotawala Ukanda wa Gaza kimetangaza uamuzi wa upande mmoja wa kusitisha mapigano, baada ya ghasia baina yake na Israel ambazo ni kubwa zaidi kwa miezi mingi. Inaarifiwa kuwa Misri ilisaidia kufikia uamuzi huo. Tangazo la makundi kadhaa ya wapalestina, Hamas ikiwemo limesema makundi hayo yatasitisha uhasama ikiwa Israel pia itaacha mashambulizi. Ghasia hizi zilianza Jumapili iliyopita kufuatia operesheni ya Israel ndani ya Ukanda wa Gaza ambamo mmoja wa makamanda wa Hamas aliuawa. Hamas ilianzisha mashambulizi ya kulipa kisasi, yaliyosababisha makabiliano yaliyouwa wapiganaji saba wa Hamas na mwanajeshi mmoja wa Israel. Israel ilishambulia Ukanda wa Gaza Jumatatu kwa kutumia ndege za kivita wakati Hamas ikivurumusha mamia ya maroketi Kusini mwa Israel. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana katika kikao cha faragha kujadili kusambaa kwa mapigano hayo lakini hakukua na maafikiano ya namna ya kuukabili.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu