Idai yapoteza makazi ya watu 400,000.

In Kimataifa

Shirika la Msalaba Mwekundu linakadiria kuwa watu 400,000 wamepoteza makaazi yao nchini Msumbiji kutokana na Kimbunga Idai kilichoipiga nchi hiyo siku tano zilizopita.

Shirika hilo limesema kiasi kidogo tu cha msaada kinaweza kuwafikia maelfu wanaouhitaji, kwa sababu mvua kubwa zinaendelea kunyesha, zikizidisha athari za mafuriko ambazo tayari ni kubwa.

Barabara, madaraja na mashamba vimesombwa na kimbunga hicho katika nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe.

Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi amesema yamkini watu 1,000 wameuawa na kimbunga hicho, na ametangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

Shirika la Chakula Ulimwenguni, WFP limesema kimbunga Idai kimepita katika eneo linalokaliwa na Wamsumbiji wapatao milioni 1.7. Watu 920,000 katika nchi jirani ya Malawi wameathiriwa pia na kimbunga hicho, pamoja na maelfu wengine nchini Zimbabwe.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu