Mkuu wa jeshi la polisi hapa nchini IGP Simon Sirro, amempongeza mkuu wa mkoa wa Lindi Bwana Godfrey Zambi pamoja na kamati yake ya ulinzi na usalama,kutokana na mkoa huo kuwa salama na kutokuwepo na matukio ya uhalifu mara kwa mara.
IGP Sirro ameyasema hayo mkoani Lindi, mara baada ya kutembelea kambi ya kikosi cha kutuliza ghasia FFU pamoja na kutembelea eneo zitakapojengwa nyumba za makazi ya askari polisi.