Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro ifikapo kesho awe ameshawaingiza askari Polisi walionguliwa nyumba zao.
Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo wakati akizindua nyumba za askari zilizojengwa mkoani Arusha.
“Nimepata mawazo ni kitu gani tunaweza kufanya kuhusu na matatizo ya nyumba za Polisi, sasa ninachoomba IGP wale walionguliwa nyumba, kesho waingie katika nyumba zao hizi mpya ambazo zimemalizwa kujengwa. Kwasababu najua muda mwingine wanaweza wakachomekwa Polisi wengine halafu waliokuwemo wakaambiwa hapana”, amesema Dkt. Magufuli.
“Sasa nataka wale wale walionguliwa ndio waingie humo kwenye nyumba kwasababu Mungu aliwasaidia, moto ukaungua ungua kwa faida ya wao lakini hii inadhihirisha ni kwa namna gani makazi ya nyumba za polisi yalivyo kuwa mabovu”.