Jacob Zuma atangaza ndoa na binti wa miaka 24.

In Kimataifa
Aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, ameushangaza umma baada ya kuwepo na taarifa za kutarajia kuoa mke wa tano, binti mdogo mwenye umri wa miaka 24.
Taarifa hizo zimethibitishwa na binti huyo ambaye ni mke mtarajiwa wa Zuma anayejulikana kwa jina la Nonkanyinso Conco, kupitia chombo cha habari cha Times live cha nchini Afrika Kusini.
“Ndio tunaoana, hayo ndiyo naweza kusema kwa sasa, nahitaji kutoa taarifa kabla sijafanya interview (mahojiano) yoyote”, amesikika binti huyo akiuambia mtandao wa Times Live.
Habari zaidi zinasema kuwa binti huyo tayari ana mtoto mchanga aliyezaa na Jacob Zuma ambaye amezaliwa siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Jacob Zuma, April 12, na tayari mahali imeshatolewa.
Jacob Zuma ambaye ana miaka 76 mpaka sasa ameshaoa mara sita, na hii itakuwa ni mara ya saba kufunga ndoa,
Tukio hilo limeonekana kuwakwaza wananchi wa Afrika Kusini na kutoa maoni yao kwenye mitandao ya kijamii, wakisema binti huyo ni mdogo sana kwa Zuma, kwani wana tofauti ya miaka 52.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu