Jaji Mutungi avionya CHADEMA na CUF

In Kitaifa

Siku chache baada ya Vyama vya Upinzani vya Chadema na CUF (Upande wa Profesa Ibrahim Lipumba), kutishiana kuharibiana kupitia oparesheni zao Mpya, Msajili wa Vyama Vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amevionya vyama hivyo.

Chadema walikuwa wa kwanza kutangaza kuingilia mgogoro ndani ya CUF wakitangaza kuanzisha ‘Oparesheni Ondoa Msaliti Buguruni’ wakilenga kumuondoa mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na ofisi ya Msajili, Profesa Ibrahim Lipumba.

Hata hivyo upande unaomuunga mkono Profesa Ibrahimu  Lipumba walijibu na kudai kuwa itakuja na ‘Oparesheni Futa Chadema’, wakilaani kitendo cha Chadema kuingilia mgogoro huo.

Kufuatia kauli hizo, Jaji Mutungi amevionya vyama hivyo kuwa vitakabiliwa na mkono wa sheria endapo vitajihusisha na vurugu ya aina yoyote.

Msajili aliongeza kuwa ingawa amesikia kupitia vyombo vya habari vitisho hivyo, hajapokea barua yoyote ya malalamiko ofisini kwake kutoka kwa vyama hivyo.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu