Kansela wa Ujerumani Angela Merkel,ametoa wito wa kubuniwa mkakati mpya wa maendeleo barani Afrika.

In Kimataifa

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel,ametoa wito wa kubuniwa mkakati mpya wa maendeleo barani Afrika.

Amesema mataifa makubwa yalioendelea kiviwanda yanapaswa kuwa tayari zaidi kupeleka silaha kuyasaidia mataifa ya Kiafrika yanayopambana dhidi ya makundi ya wanamgambo.

Merkel pia ameisifu ujasiri wa mataifa ya Afrika ambayo yanashiriki katika mapambano dhidi ya wanamgambo wa Kiislamu nchini Mali na mataifa jirani.

Ameongeza kuwa Ujerumani itaunga mkono juhudi za Ufaransa kulishinikiza baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuidhinisha kikosi cha Afrika Magharibi kupambana na ugaidi na usafirishaji haramu wa binadamu katika eneo la Sahel.

Kiongozi huyo wa Ujerumani pia ametangaza mipango ya mapatano kati ya kundi la mataifa ya G20 na bara la Afrika, ambayo yanaondokana na mfumo wa zamani wa misaada ya kimaendeleo na badala yake kujikita katika fursa za ushirikiano na mataifa ya Afrika, ambayo mengi yanashuhudia viwango vikubwa vya ukuaji wa kiuchumi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu