Kesi ya Aveva na Kaburu yapigwa kalendaa.

In Kitaifa

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeahirisha kesi ya utakatishaji fedha ya USD 300,000, inayowakabili Rais wa klabu ya Simba Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange, hadi November 10 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.
Wakili wa Serikali Vitalis Peter amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu Victoria Nongwa kuwa, kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika, pia ameeleza uchunguzi wa kesi hiyo unaendelea na jalada la kesi bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Baada ya kueleza hayo Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi November 10 2017, na watuhumiwa kurudishwa rumande.
Evans Elieza Aveva na makamu wake Geofrey, wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu