Kijiji cha Ilkereni kata ya Kisongo jijini Arusha kinakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji jambo linalopelekea wanafunzi wa shule ya msingi kushindwa kufanya vizuri kitaaluma
Akizungumza na vyombo vya habari mwalimu mkuu msaidizi wa shule hiyo Evarist Mtei Lokisa amesema kuwa changamoto ya maji katika eneo hilo limekuwa sugu na hivyo kuiomba serikali kulichukulia hatua
Kinamama wa kijiji hicho ambao ndo waanga wakubwa kwenda umbali mrefu kutafuta maji na kuacha shughuli zao, wamepaza sauti zao huku ambapo wamesema wanashindwa kuendelea na shughuli zao za ujasiriamali kwa kwenda umbali mrefu kutafuta mahi
Mtendaji wa kata hiyo, Bwn Brison Mwandi amesema kuwa maji yanayopatikana kijijini hapo yanatokana na mvua na hiyo inasababisha kutokuwa na usalama wa afya zao, hivyo amepaza sauti kwa idara husika ambapo kwa sasa wameanza utekelezaji wa miradi ya mabomba ya maji
Mara baada ya changamoto hiyo kusota kipindi kirefu katika eneo hilo wadau mbalimbalu wamejitokeza kutoa msaada kadri ya uwezo wao ambapo kampuni ya uuzaji wa viwanja na mashamba HARIZONA iilyopo jijini Arusha imejitolea matank 2 ya maji kwenye vyoo vipya vya matundu 8 Hamrey Ndosi