kilichojiri Mahakamani kesi ya Escrow.

In Kitaifa
Mwendesha Mashitka wa Takukuru, Leornad Swai ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mmiliki wa IPTL Harbinder Singh Sethi anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha ameomba madaktari wake kutoka Afrika Kusini wawepo wakati akifanyiwa upasuaji wa puto.
Pia Swai ameeleza kuwa Mfanyabiashara James Rugemarila hana ugonjwa wa saratani, pia na yeye ameomba madaktari wake kutoka India wawepo wakati akiwa anafanyiwa uchunguzi.
Swai ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipoitishwa kwa ajili ya kutajwa ambapo upelelezi bado haujakamilika.
Wakili Swai alieleza kuwa taarifa kuhusu afya za washtakiwa alizipata magereza January 17, 2018 kama mahakama ilivyoamuru azifatilie.
Swai alidai mshtakiwa Sethi anaishi na puto tumboni ambalo limeisha muda wake, ambapo madaktari wa Muhimbili wamesema linatakiwa liondolewe.
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba alisema inaonekana madaktari wa Sethi wameruhusiwa kuja nchini kumtibia, hivyo Magereza wafanye utaratibu kama uliotumika kwa Sethi ili na Rugemarila atibiwe na madaktari wake.Kesi imeahirishwa hadi February 2,2018.
Kwa pamoja washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh.Bil 309.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu