Kocha wa simba kuwaboreshea mikataba wachezaji wake.

In Michezo

KOCHA Mkuu wa Simba Mbelgiji, Patrick Aussems amepanga kuwaboreshea mikataba baadhi ya wachezaji wake wazawa kwa sharti awe amecheza nusu ya mechi za Ligi Kuu Bara na michuano mingine waliyoshiriki.

Kati ya wachezaji waliopendekezwa kuboreshewa mikataba yao ni viungo wa timu hiyo, Said Ndemla na Mohamed Ibrahim ‘Mo’ ambao wote hivi karibuni walikuwa wanatajwa kuwaniwa vikali na Yanga.

Ndemla yeye mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu huku Mo akibakisha mwaka mmoja ambaye alikuwa anatajwa kutolewa kwa mkopo.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumamosi, kocha huyo amefi kia hatua ya kuboresha mikataba ya wachezaji hao kutokana na kutovutiwa na viwango vya wachezaji wazawa.

Mtoa taarifa huyo alisema, kama kungekuwepo na wachezaji wazawa wenye uwezo kushinda alionao hivi sasa, basi angefanya usajili hivyo amependekeza kuendelea na wachezaji hao katika msimu ujao.

“Ukiangalia viwango vya wachezaji wazawa waliopo kwenye timu nyingine hakuna waliowazidi waliopo Simba, hiyo ndiyo sababu kubwa inayomfanya kocha apendekeze kubaki nao na waboreshewe mikataba kwa wale ambao mikataba yao inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu.

“Kocha anataka mchezaji mpya atakayesajiliwa Simba awe na uwezo mkubwa utakaompa changamoto mchezaji atakayemkuta siyo asajiliwe halafu akae benchi,” alisema sosi huyo.

Alipotafutwa Aussems alisema: “Tangu msimu huu wa ligi umeanza sijaona mchezaji mzawa aliyenivutia nimsajili. Nimependekeza kwa uongozi kuwaboreshea baadhi ya wachezaji mikataba yao kwa wale ambao inamalizika mwishoni mwa msimu.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu