Korea Kaskazini yaonya kuhusu shughuli za kijeshi la Korea Kusini kwenye eneo lake- KNCA

In Kimataifa

Korea Kaskazini imesema ilikuwa inautafuta mwili wa raia wa Korea Kusini aliyeuwawa na wanajeshi wake, lakini ikionya kwamba shughuli za kijeshi za Korea Kusini zilitishia kuongezeka kwa wasiwasi. 

Kulingana na shirika la habari la habari la Korea Kaskazini, KNCA hii leo mamlaka za nchini humo zilikuwa zinazingatia namna ya kuukabidhi mwili huo kwa Korea Kusini iwapo utapatikana. 

Ripoti ya KNCA ililiita tukio hilo kuwa ni baya na ambalo halikutakiwa kutokea ingawa ilionya kwamba shughuli za kijeshi za Korea Kusini karibu na eneo kulikotokea tukio hilo zilikuwa zimevuka na kuingia kwenye eneo la maji ya Korea Kaskazini na kutaka kusimamishwa kwa shughuli hizo ili kuepusha hali ya wasiwasi. 

Msemaji wa wizara ya ulinzi ya Korea Kusini alipoulizwa alisema hawezi kuzungumzia tuhuma hizo za Korea Kaskazini kwa sasa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu