KRC Genk yatwaa ubingwa wa Ubelgiji.

In Kimataifa, Michezo

KRC Genk imetwaa ubingwa wa Ubelgiji kwa mara ya nne.

 

KRC Genk imetwaa ubingwa wa Ubelgiji kwa mara ya nne, ikiwa ni miaka 20 tangu walipotwaa ubingwa huo kwa mara ya kwanza (1999), na miaka 8 tangu walipoutwaa kwa mara ya mwisho (2011). K.R.C Genk timu anayochezea nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta imetwaa taji la ligi ya soka ya Ubelgiji baada ya kutoka sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Anderlecht na kufikisha pointi 51 ambazo hazitafikiwa na timu nyingine.

Ubingwa huo umepatikana baada ya mahasimu wao Club Brugge kupoteza mchezo wao kwa kipigo cha mabao 2-0 mbele ya Standard Liege hivyo kupoteza uwezo wa kufikisha pointi 51 huku ukiwa umebaki mchezo mmoja katika mchuano wa timu sita bora.

Samatta ambaye anaongoza kwa ufungaji mabao kwenye ligi hiyo alianza mchezo huo kabla ya kupumzishwa kwenye kipindi cha pili.

Kwa ubingwa huo Genk wamepata nafasi ya kucheza michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu