Kufuatia utafiti uliobaini uwepo wa mashapo ya madini aina ya Bunyu (grafait) tani 689.7 milioni katika mikoa ya Lindi na Mtwara, wananchi wa kata ya Chiwata wilayani Masasi mkoani Mtwara wanaozunguka mradi wa mgodi wa madini hayo wameiomba serikali kusimamia viwango vya malipo ya fidia kutokana na thamani ya ardhi na wanavyonufaika nayo.

In Kitaifa
Kufuatia utafiti uliobaini uwepo wa mashapo ya madini aina ya Bunyu (grafait) tani 689.7 milioni katika mikoa ya Lindi na Mtwara, wananchi wa kata ya Chiwata wilayani Masasi mkoani Mtwara wanaozunguka mradi wa mgodi wa madini hayo wameiomba serikali kusimamia viwango vya malipo ya fidia kutokana na thamani ya ardhi na wanavyonufaika nayo.
Katika mkutano maalum wa hadhara uliotishwa na wananchi hao ulioshirikisha mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na kampuni ya utafiti ya Nachi Resources wameiomba serikali kuangalia upya viwango vya malipo ya uthamini wa ardhi yao iliyogundulika kuwa na madini ya grafait ambayo hutumika katika kutengeneza Betri zinazotumika katika magari, simu, tochi pamoja na kuzalisha penseli.
Kufuatia hali hiyo iliyotawala mkutano huo ikiwemo ujumbe wa mabango kutoka kwa wananchi ,Mbunge wa jimbo la Ndanda pamoja na mtafiti wa mradi huo kutoka kampuni ya Nachi Resources wamezungumzia madai ya wananchi hao na kutolea ufafanuzi.
Madini ya grafait ama bunyu yamegundulika katika vijiji vya chiwata na chidya katika mkoa wa Mtwara ambapo kwa mkoa wa lindi yamegundulika katika vijiji vya Chunyu, Mihewe, Matambalale, Chikwale, Namikulo, Chiundu, Nagulugai wilayani Ruangwa na kwenye kata ya Namangale wilayani humo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu