Kufuatia malalamiko ya baadhi ya wadau wa soka kuhusu
kufanya vibaya kwa baadhi ya waamuzi wa ligi kuu
Tanzania bara na ligi daraja la kwanza wakihoji uwezo
wao kitu ambacho kinapelekea soka la Tanzania kupoteza
mwelekeo
Kocha wa AFC ya Arusha timu inayoshiriki ligi Daraja la
kwanza Ulimboka Mwakwingwe, pia kwa upande wake ametoa maoni kuhusu Waamuzi
“Waamuzi wana kamati zao Waamuzi wana Chama chao kwahiyo kuna Mwenyekiti kuna Katibu wao ndiyo wanafanya utaratibu wote wa Marefa katika kupanga kwenye mechi na michezo mingine yote, kwa hiyo wao kama wao wanazungumza na marefa wao juu ya malalamiko yanayotokea kwa wadau, walimu na vilabu mbalimbali kwahiyo mimi naimani wakikaa chini watafanya vile inavyotakiwa.” – alisema Ulimboka Mwakingwe