Ligi ya Ujerumani-Bundesliga inaanza tena leo, na kuifanya kuwa ligi kubwa ya kwanza barani Ulaya ambayo ilisitishwa, ikiwa ni miongoni mwa jitihada za kukabiliana na janga la corona. Asasi yenye dhamana na ligi hiyo DFL, ilimshawishi Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel na viongozi wa majimbo kuruhusu kufanyika kwa mchuano huo, kwa makubaliano ya kufanya jitihada za hali ya juu za kudhibiti maambukizi. Kabumbu itasakatwa viwanja vikiwa vitupu. Ujerumani ikabiliwa na janga la corona huku ikiwa na vifo vichache, ikilinganisha na mataifa mengine ya ulaya lakini suala la mikusanyiko bado ni la hatari. Miongoni mwa mechi zitakazovuta wengi ni Borussia Dortmund na Schalke 04. Kwa kawaida mchuano huko unavutia umma watu 82,000 uwanjani lakini safari hii uwanja utakuwa mtupu. Jumapili Bayern Munich itafuana na Union Berlin.