Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeifutia kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleao (Chadema) Tanzania Bara, Tundu Lissu na wenzake watatu.
Ni baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa hao.
Lissu na wenzake walikuwa wanakabiliwa na mashtaka matano likiwemo la kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002, katika kesi ya jinai namba 208/2016.
Mbali na Lissu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni waliofutiwa mashtaka yao na kuwa huru ni Jabir Idris, Mhariri wa Gazeti la Mawio, Simon Mkina, Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboo.