Maafande wa Jeshi la polisi Tanzania leo Oktoba 2, 2019 wamekamilisha maandalizi yao wakiwa jijini Dar es salaam chini ya kocha Suleyman Matola.
Polisi Tanzania kwa siku kadhaa wamekua jijini humo wakifanya maandalizi ya kuelekea mchezo wao kesho dhidi ya Young Africans, na wanaamini watakua na kila sababu ya kuibuka na ushindi kama walivyofanya walipocheza mchezo wa kirafiki kwezi Agosti mjini moshi mkoani Kilimanjaro.
Kocha Suleyman Matola amezungumza na vyombo vya habari kuelekea mpambano ho wa kesho ambao utarindika katika uwanja wa Uhuru, Dar es salaam, na kusema kuwa kikosi chake kipo katika hali nzuri na anakiamini kitapambana wakati wote na kufanikisha azma ya kuibuka na ushindi.