Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli, amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge, abadilike na kuachana na upole badala yake awe mkali kwa lengo la kuhakikisha miradi ya jiji hilo inaenda vizuri.
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo hii leo Oktoba 8, 2020, jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wakazi wa jiji hilo kwenye zoezi la kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani kilichopo maeneo ya Mbezi Louis ambacho ujenzi wake umekamilika kwa 85%.
“Wahandisi wa mikoa na wilaya hamieni hapa msimamie huu mradi kwa hiyo uongozi wa mkoa, ninajua mkuu wa mkoa wewe ni mgeni hapa lakini badilika uwe mkali usiwe sheikh au Askofu, ni lazima watu watimize wajibu wao, muondoa ‘damage’ ambayo iko kwenye mkataba”, amesema Rais Magufuli.