Majaliwa aagiza mawaziri wakutane kuondoa mkanganyiko kwenye vyombo vya udhibiti hapa nchini.

In Kitaifa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu, Bibi Jenista Mhagama akutane na mawaziri wa sekta nyingine na watafute namna ya kuondoa mkanganyiko uliopo kwenye vyombo vya udhibiti hapa nchini.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Bungeni jijini Dodoma, kwenye mkutano wa 15 wakati akihitimisha hoja ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2019/2020.

Amekuwa akitoa ufafanuzi juu ya masuala yaliyogusa vyombo vya udhibiti kama vile Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA, Shirika la Viwango Tanzania TBS, Mkemia Mkuu wa Serikali, Mamlaka nyingine za udhibiti pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, OSHA, BRELLA na Taasisi ya Mionzi ambayo yaligusiwa na Waheshimiwa Wabunge.

Amesema licha ya Serikali kujenga mazingira wezeshi na rahisi ya kufanya biashara na uwekezaji, bado kumekuwepo na malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara na wawekezaji kama walivyoeleza Waheshimiwa Wabunge wakati wa kuchangia hoja hiyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu