Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula, kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka serikalini.

In Kitaifa

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kamwe Serikali haitagawa chakula, kwa wananchi wavivu ambao hawataki kufanya kazi na kusubiri chakula kutoka serikalini.

Ametoa kauli hiyo wakati akihutubia mamia ya wananchi wa Manispaa ya Musoma ,katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mukendo mjini humo.

Samia amesisitiza kuwa Serikali itapeleka chakula kwa wananchi ambao mazao yao yaliharibiwa kwa mvua, au yalikauka kwa ukame au kwa maafa mengine ,na sio kwa wananchi wanaokaa vijiweni mchana kutwa bila kufanya kazi wakisubiri neema ya chakula kutoka kwa Serikali.

Amewahimiza wananchi kote nchini kuendelea kufanya kwa bidii ikiwemo shughuli za kilimo, na pindi wanapovuka wajiwekee akiba na waache tabia ya kuuza mazao yote wanayovuna, ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa chakula kwenye familia zao.

Pia aliwataka viongozi wa mkoa wa Mara washirikiane na wananchi katika kuwaelemisha mbinu bora za kilimo ili waweze kupata mazao mengi ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu