Makonda kutengeneza ajira vikundi vya kukimbia (jogging club).

In Kitaifa
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, ametangaza mpango kabambe wa kuviwezesha vikundi vya mazoezi ya kukimbia (jogging club) kwa kuweka utaratibu wa mashindano ya kila mwisho wa mwezi.
Ambapo kikundi kitakachoshinda kitapatiwa kiasi cha shilingi milioni 10 kama mtaji wa kufanya shughuli za kujikwamua kiuchumi.
Hatua hiyo imekuja baada ya Makonda kubaini idadi kubwa ya vijana hao wakimaliza mazoezi asubuhi hawana shughuli ya kufanya hivyo wanakaa vijiweni.
”Vijana wengi wa ‘Jogging Club’ hizo wanafanya mazoezi asubuhi halafu hawana kazi za kufanya wanarudi vijiweni, hiyo si salama maana unaweza ukashangaa wakajikuta wameanza kuwa na ‘speed’ kubwa na matokeo yake wakapita na mikoba ya wakina mama kama hawana kazi za kufanya.
Ameongezea ”Kwa hiyo sisi tunaratibu na kupitia hadhara hii niwaambie wananchi kwamba tunapanga mipango kwa kila mwisho wa mwezi kuwepo na mashindano ‘Jogging Club”, amesema Makonda.
Amesema kitendo cha kukaa kijiweni kinaweza kuwasababishia kushawishika kufanya vitendo vya uhalifu hivyo kwa kuwapatia mtaji itawawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali utakaowakwamua kiuchumi.
Amesema mashindano hayo yataanza rasmi mwezi ujao, na kwa kuanzia shindano hilo litaanzia wilaya ya Temeke kwa kuwa ndiyo inayoongoza kwa Jogging Club, kwa Dar es salaam, hivyo amezitaka jogging club zote za mkoa kukutana Temeke.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu