Mama Salma Kikwete amuhusia Alikiba na mkewe.

In Kitaifa

Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete amewaasa wasanii wawili wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba na mdogo wake Abdu Kiba kuwa wawe waaminifu kwenye maisha yao ya ndoa hasa hasa kwenye masuala ya simu.

Mama Salma Kikwete akiwaasa jambo Alikiba na mkewe

Mama Salma ametoa wosia huo jana Aprili 29, 2018 katika hoteli ya Serena  jijini Dar es salaam kwenye sherehe za harusi ya Alikiba na mdogo wake Abdukiba ambao wote wamefunga ndoa wiki mbili zilizopita.

Simu mtihani na ni hatari, mkiendekeza simu mnachukua mnaangalia mtaaachana kabla ya siku si nyingi. Aminianeni mkiaminiana  maisha yatakuwa mazuri, laikini kila dakika ukirudi basi umerudi unaanza kupakua nani ametuma meseji, hapana. Wakati mwingine simu inalia ikishalia ile simu unakosa amani ya moyo unatoka nje au unaingia chooni kuongea,“amesema Mama Salma Kikwete.

Kwa upande mwingine Mama Salma Kikwete amesema yeye tangu afunge ndoa na Mzee Kikwete wamekuwa wakichangia simu na mara nyingine hata kupokeleana pale inapokuwa inaita.

Alikiba na mdogo wake Abdukiba wamefunga ndoa wiki mbili zilizopita ambapo Alikiba alifunga ndoa na mchumba wake Aminah Khalef jijini Mombasa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu