Mambo 9 ya msingi ya kuzingatia ili kuwa dereva bora barabarani

In Kitaifa

Ajali si kitu cha kuzoeleka, lakini ni rahisi sana kuepuka ajali barabarani kwa kuzingatia
sheria na kanuni za barabarani, mara nyingi ajali nyingi husababishwa na uzembe
mdogo mdogo unaofanywa na madereva ambao hujiona ni madereva bora kuliko
dereva mwingine yeyote aliyopo barabarani.
Madereva wengi wenye uzoefu wa kuendesha barabarani hujikuta wakijiamini kupita
kiasi huku madereva ambao bado si wazoefu barabarani hujikuta kuwa makini haswa,
jambo ambalo ni zuri na muhimu kuzingatiwa na dereva yeyote aliyopo barabarani
kwani.
Kupokea simu, kuchat kwa njia ya meseji, kusinzia au kuendesha gari ukiwa umelewa
ni mambo ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele sana kwani yamekuwa kwa kiasi
kikubwa yakisabisha ajali mbalimbali barabarani hata kanuni na sheria za usalama

barabarani imekuwa ikikemea vikali sana tabia hizo na kusisitiza zaidi madereva
kufuata kanuni za barabarani lengo likiwa ni kuepusha ajali zaidi.
Hapa chini nimekuwekea mambo makubwa na ya msingi 9 ambayo yanaweza
kukusaidia na kukufanya kuwa dereva mzuri unapokuwa barabarani.

  1. Angalia Mbele: Hapa tunazungumzia madereva waopenda kuendesha gari huku
    wakiwa wanatumia sim au kugeuka geuka nyuma au maongezi na abiria wako. Mambo
    hayo na yanayofanana na hayo yanaweza kumtoa dereva kwenye utulivu wa barabara
    na hivyo inapotokea dharula kama watumiaji wengine kukatiza ghafra mbele yake
    huweza kusababisha ajali.
  2. Usiisogelee sana gari ya mbele yako. Zaidi tunaongelea gari inapokua kwenye
    mwendo, ambapo imekua jambo la kawaida kwa madereva wengine kuwasogolea sana
    wenzao bila kujali dharula inayoweza kumpata huyo wa mbele kama kufunga break za
    ghafra au kupasukiwa tairi jambo linaloweza kusababisha ajali hiyo ikukumbe na wewe
    kwa kua uwezekano wa kukimudu chombo ukiwa kwenye mwendo na karibu zaidi ya
    mwenzio wa mbele ni mdogo.
  3. Epuka Break za ghafra. Matumizi ya break za ghafra iwe ni chaguo la mwisho, lakini
    muhimu ni kuhakikisha unakadiria barabara yako na hivyo ushike break taratibu. Iwapo
    utashika kwa ghafra huku gari ya nyuma yako ikiwa imekufata kwa karibu kuna
    uwezekano wa kutokea ajali. Mara nyingi hili linatokea kwa madereva wanapoamua
    ghafra kusimama kwenye zebra ili watembea kwa miguu.
  4. Gia ya Manual. Watanzania walio wengi tunaotumia gari binafsi hatufahamu namna
    ya kutumia gari zenye gia ya manual, badala yake tumezoea Automatic, lakini dereva
    mzuri ni yule anayejifunza kutumia gia za aina zote yaani Manual na Automatic kwa kua
    faida ya Manual ni kua inachangia kwenye matumizi madogo ya mafuta, lakini pia
    humuongezea dereva ujuzi zaidi awapo barabarani kwa kua kila kitu anakifanya yeye
    mwenyewe manually. Zaidi wakati wa dharula dereva hatohitaji aje dereva mwingine
    kutoka mbali aendeshe hilo gari manual bali yeye mwenyewe ataingia na kuendesha
    gari hilo.
  5. Usikae upande uwapo kwenye usukani. Baadhi ya madereva hukaa upande kwenye
    magari yao jambo linalowafanya kujisahau na kukanyaga mafuta badala ya break au
    break badala ya mafuta au mda mwingine kujikuta akikanyaga vyote kwa pamoja hali
    inauoweza kusababisha ajali. Na kwa safari ndefu mkao wa upande utamfanya dereva
    ahisi maumivu ya mgongo au kiuno. Inaushiliwa kukaa kwa kunyooka kwenye usukani
    na kurelax mwili huku ukiwa makini na watumiaji wengine wa barabara.
  6. Kurudi nyuma. Hili ni tatizo kubwa kwa akina mama wengi na baadhi ya wababa pia.
    Ni muhimu kujifunza kwa kufanya mazoezi ya kurudisha gari yako nyuma bila kuhitaji
    msaada kwa kua kuna siku utahitaji msaada utakosa na hivyo unaweza kuligonga gari
    lako kwa kushindwa kufanya makadirio mazuri kwa kutumia vioo vyako ya pembeni na
    ndani, unapoona unashindwa kabisa kutumia vioo basi geuza shingo ili kuweza kufanya
    hayo makadirio na kuona vizuri nyuma.
  7. Kuegesha gari. Kwa sasa kwenye miji mikubwa kuna majengo ya kisasa ya parking
    ambazo zinakua zimebanana na hivyo kuwapa uoga baadhi ya madereva kupaki gari
    katikati ya magari mengine kwa kuhofia kugonga. Hili nalo tunashauliwa tuweke uoga
    pembeni tujiamini na kufanya mazoezi taratibu na kwa tahadhari mpaka tutazoea.
    Haipendezi unaingia kupaki unaomba msaada kwa mtu mwingine akuingizie gari hiyo
    kwenye parking husika.
  8. Kuegesha gari katikati ya gari zinafuatana. Hili ni tatizo kubwa kwa madereva wengi
    kwa kua kukadiria kwetu ni tatizo na hali ya kutojiamini. Njia nzuri ya kupaki gari katikati
    ya gari zilizofuatana ni kuingia kwa rivasi. Ikiingia kwa rivasi uwezekano wa kupaki gari
    ikiwa imenyooka ni mkubwa kuliko kuingia kwa mbele inaweza kusababisha sehem ya
    nyuma ibaki upande wa barabarani.
  9. Uvumilivu. Tunatakiwa kua wavumilivu kwenye uzurmbe unaofanywa na madereva
    wengine kwa kua ukiruhusu hasira ikutawale unaweza kujikuta unafanya mambo ya
    ajabu na ukapata matatizo hapo barabarani. Mfano umekwazuraza na gari ya pembeni
    yako inatakiwa uelewe kwamba ajali zipo kwa mtu yoyote anayetumia barabara hivyo
    iwapo mtu kakugusa bahati mbaya lazima utumie busara kuzungumza naye na
    kuyamalizq badala ya kutumia nguvu na matusi. Hii piq kwa wale ambao kukiwa na
    foleni kidogo wanapiga honi akiona haitoshi anamfaya mwenzie kumtukana, hili pia si
    jema na unaweza kupata matatizo ambayo hukuyategemea iwapo utakutana na mtu
    mkorofi zaidi yako

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu