Kuelekea sikukuu ya wafanyakazi duniani Mei Mosi 2021 rais
washirikisho la vyama cha wafanyakazi Tanzania TUCTA
Tumaini Nyamhokya amesema miongoni mwa mambo
wanayoyatarajia katika serikali ya awamu ya sita inayoongozwa
na Rais Samia Suluhu Hassan ni nyongeza ya mishahara.
Nyamhokya ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Tabora alipofika
kukagua ujenzi wa ofisi ya chama cha wafanyakazi wa serikali
za mitaa TALGWU mkoa zinazojengwa kupitia makusanyo
kutoka kwa wanachama.