Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania (CHADEMA), Freeman Mbowe leo Novemba 19, 2019 amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam akipatiwa matibabu,mdhamini wake katika kesi ya uchochezi inayomkabili Kiongozi huyo pamoja na Viongozi wengine 8 wa chama hicho, Greyson Selestine ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.