Mbowe na wenzake, Halima Mdee wapata dhamana.

In Kitaifa

Viongozi Sita wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamaeachia huru mara baada ya kutimiza masharti ya dhamana Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.

Washtakiwa hao walitakiwa kila mmoja kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini hati ya dhamana ya Tsh Milioni 20 na kuwa na barua kutoka kwa viongozi wao wa vijiji au mtaa ambao watapaswa kuwa na nakala za vitambulisho vyao.

Viongozi hao waliopata dhamana ni  Freeman Mbowe, John Mnyika , Ester Matiko, Salum Mwalimu, Peter Msigwa na Dkt. Vicent Mashinji.

Katika hatua nyingine Mbunge wa Kawe, Halima Mdee ameunganishwa na  akina Freeman Mbowe ambapo alisomewa mashtaka mawili ya kufanya mkusanyiko usio halali na kuendelea na mkusanyiko huo, kutotii amri iliyowataka kutawanyika na kusababisha vurugu iliyosababisha kifo cha Akwilina Akwilini na askari kujeruhiwa.

Hata hivyo naye Mahakama imempa dhamana kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini kwa maandishi bondi ya Sh milioni 20 na kuripoti mara moja kila wiki.

JIUNGE NA BONGO5.COM SASA

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu